Listen "Nafsi Yangu Ina Amani"
Episode Synopsis
Nafsi Yangu Ina Amani
Katika dunia ambayo inashangalia ukamilifu wa mwanaume, dunia ambayo bado haiko tayari kuzungumzia kwa kina juu ya afya ya akili ya mwanaume, dunia ambayo mwanaume anayepitia changamoto za afya ya akili bado anatengwa na kuonekana mtu asiyefaa kushirikishwa na jamii yake, Sunday Kapesi anapambana kubadilisha hayo.
Toka safari yake ya kuondokewa na baba yake mzazi, kuanza kuingia kwenye matumizi ya madawa ya kulevya na kupata urahibu, kuweza kumuangalia mama yake na ndugu zake usoni na kukiri kwamba anahitaji msaada, na kuamua kwenda “rehab” ili aweze kupambana na urahibu huo, Sunday haachi simulizi yeyote kwenye mazungumzo haya.
Kama baba, kama mtoto, kama kaka, na kama mtu ambaye ana ndoto za kuisaidia na kuiokoa jamii yake, Sunday anaongea na sisi ni namna gani ni rahisi mno kwa mtu yeyote, hususani mwanaume kuingia kwenye urahibu, lakini pia anatutia moyo kwamba kila tatizo bado linauwezo wa kutatuliwa.
Ilimchukua muda kiasi gani kwa Sunday kupambania afya yake ya akili mpaka kufikia hatua ya kuweza kupata “amani kwenye nafsi yake”?
Sikiliza kiundani mazungumzo haya ili na wewe uweze kufahamu kwamba haijalishi unapitia magumu kiasi gani, siku zote kuna suluhisho la unayopitia, na linaweza kuwa suluhisho bora ambalo litajenga zaidi afya yako ya akili na kukufanya uwe bora zaidi ya jana. Pambana kuipa nafsi yako amani
Katika dunia ambayo inashangalia ukamilifu wa mwanaume, dunia ambayo bado haiko tayari kuzungumzia kwa kina juu ya afya ya akili ya mwanaume, dunia ambayo mwanaume anayepitia changamoto za afya ya akili bado anatengwa na kuonekana mtu asiyefaa kushirikishwa na jamii yake, Sunday Kapesi anapambana kubadilisha hayo.
Toka safari yake ya kuondokewa na baba yake mzazi, kuanza kuingia kwenye matumizi ya madawa ya kulevya na kupata urahibu, kuweza kumuangalia mama yake na ndugu zake usoni na kukiri kwamba anahitaji msaada, na kuamua kwenda “rehab” ili aweze kupambana na urahibu huo, Sunday haachi simulizi yeyote kwenye mazungumzo haya.
Kama baba, kama mtoto, kama kaka, na kama mtu ambaye ana ndoto za kuisaidia na kuiokoa jamii yake, Sunday anaongea na sisi ni namna gani ni rahisi mno kwa mtu yeyote, hususani mwanaume kuingia kwenye urahibu, lakini pia anatutia moyo kwamba kila tatizo bado linauwezo wa kutatuliwa.
Ilimchukua muda kiasi gani kwa Sunday kupambania afya yake ya akili mpaka kufikia hatua ya kuweza kupata “amani kwenye nafsi yake”?
Sikiliza kiundani mazungumzo haya ili na wewe uweze kufahamu kwamba haijalishi unapitia magumu kiasi gani, siku zote kuna suluhisho la unayopitia, na linaweza kuwa suluhisho bora ambalo litajenga zaidi afya yako ya akili na kukufanya uwe bora zaidi ya jana. Pambana kuipa nafsi yako amani
More episodes of the podcast Men The Podcast
Jembe Kazini, Mpweke Nyumbani
21/10/2025
Wanaume vs Pombe: Tunaishi au Tunaisha?
07/10/2025
Mimi Nilivyo, Natosha
29/07/2025
Bado Najifunza
15/07/2025
Bro, Upo Tayari kuwaunga Mkono Wanawake?
01/07/2025
Hili Nalo Litapita
04/06/2025
Jikubali, Jipende
20/05/2025
Embracing The Legacy, Creating My Own Path
06/05/2025
100 Episodes later, Bado Tunapambana
23/04/2025
Kamari ni stress
09/04/2025
ZARZA We are Zarza, the prestigious firm behind major projects in information technology.